BERLIN: Bunge la Ujerumani laidhinisha ndege zipelekwe Afghanistan
9 Machi 2007Matangazo
Bunge la Ujerumani, Bundestag, limeidhinisha uamuzi wa serikali wa kutuma ndege sita aina ya tornado kwenda nchini Afghanistan na kuongeza wanajeshi 500 zaidi nchini humo.
Mpango huo ulikosolewa vikali na wanasiasa wa upinzani.
Ndege za tornado zitatumiwa kupigia picha maeneo wanakojifidha waasi wa Taliban na kuliwezesha jeshi la ISAF linaloongozwa na shirika la kujihami la kambi ya magharibi NATO kupanga operesheni zake.