1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BERLIN: Shirika la Watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF limekumbusha juu ya hali...

26 Novemba 2003

mbaya za mayatima wa ukimwi barani Afrika, na wanahitaji msaada wa haraka. Idadi ya mayatima waliondokewa na wazazi wao kwa sababu ya ukimwi, hivi leo ni millioni 11, na idadi itapanda marudufu kukaribia millioni 20 ufikapo mwaka 2010, - alisema mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa mwenye kuhusika na Ukimwi barani Afrika, Joseph Lewis, mjini Berlin. Kutokana na siku ya Ukumbusho wa Ukimwi Duniani, Jumatatu ijayo, aliwasilisha ripoti ya shirika la UNICEF juu ya hali za mayatima wa ukimwi barani Afrika.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW