1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BERLIN:Kansela Merkel aitaka Uturuki kuitambua Cyprus na kukubali biashara huru

6 Novemba 2006

Kansela Angela Merkel wa Ujerumani amesema Uturuki lazima ichukue hatua katika mzozo wake na Umoja wa Ulaya juu ya kuitambua na kufanya biashara huru na Cyprus ambayo ni mwanachama wa Umoja huo.

Ujerumani inaitaka Uturuki kuiondolea vikwazo vya kibiashara Cyprus lakini Uturuki badala yake inataka vikwazo vilivyowekwa na shirika la biashara duniani WTO dhidi ya Cyprus kaskazini inayodhibitiwa na Uturuki viondolewe kwanza.

Uturuki imekataa kuitambua serikali ya Cyprus ya Ugiriki ambayo kimataifa inawakilisha kisiwa hicho katika Umoja wa Ulaya.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW