1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Biden aanza ziara yake ya kwanza ya kigeni

10 Juni 2021

Rais Joe Biden ameanza ziara yake ya kwanza ya kigeni tangu aingie madarakani kwa kusifia kujitolea kwa Marekani katika jumuiya ya kujihami ya NATO na kutuma onyo kali kwa Urusi wakati akiwa Uingereza

Großbritannien Vor dem G7-Gipfel in Cornwall - Joe Biden, Präsident der USA
Picha: Patrick Semansky/PA Wire/dpa/picture alliance

Akiwahutubia karibu wanajeshi 1,000 na familia zao katika Kituo cha Jeshi la Anga cha Uingereza, Biden amesema atawasilisha ujumbe wa wazi kwa Rais wa Urusi Vladmir Putin watapokutana wiki ijayo baada ya kuhudhuria mikutano tofauti ya kilele na NATO na G7 na viongozi wa UIaya.

Biden amesema amedhamiria kuyajenga upya mahusiano ya Marekani na Ulaya na kurekebisha mahusiano na Urusi baada ya miaka minne migumu chini ya Rais Mrepublican Donald Trump, ambaye maamuzi yake ya kuongeza ushuru kwa bidhaa na kujiondoa kwenye mikataba yaliharibu mahusiano na washirika wakuu. Biden atakuwa Uingereza hadi Jumapili

Kwa washirika wengi wa Marekani, Biden ni kiongozi wanayemtazama kwa jicho la faraja. Na sababu kubwa ni kwamba mtangulizi wake alisababisha mvurugano mkubwa mara kwa mara,akiushutumu muungano wa kijeshi wa NATO kwamba umekuwa ukiitumia vibaya Marekani, na kuitukana Umoja wa Ulaya, na wakati mmoja kufikia hatua mpaka ya kuondoka kwenye mkutano wa kilele wa G7 uliofanyika Canada mwaka 2018.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW