1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Biden asema Netanyahu anakwamisha mapatano Gaza

2 Septemba 2024

Rais wa Marekani Joe Biden amesema Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu hafanyi vya kutosha kuhakikisha makubaliano yanafikiwa juu ya kuachiwa kwa mateka wa Israel wanaoshikiliwa na Hamas katika Ukanda wa Gaza.

Israel Tel Aviv | Joe Biden
Rais Joe Biden amekuwa akijaribu kuratibu makubaliano ya kusitisha vita Gaza lakini anasema Netanyahu anarefusha vita hivyo kwa maslahi binafsi.Picha: Evan Vucci/AP Photo/picture alliance

Rais Joe Biden wa Marekani amesema hii leo kwamba anakaribia kuwasilisha pendekezo la mwisho la makubaliano ya kuachiliwa mateka wanaoshikiliwa na Hamas katika Ukanda wa Gaza na kusema hadhani kama Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu anafanya vya kutosha kufikia makubaliano hayo.

Biden alikuwa akizungumza na waandishi wa habari katika Ikulu ya White House siku mbili baada ya vikosi vya Israel kusema vimegundua miili sita ya mateka kwenye handaki huko Gaza.

Israel yazidisha mashambulizi katika ukanda wa Gaza

01:35

This browser does not support the video element.

Soma pia: Hamas yasema Biden anaipa Israel "Tiketi" ya kuendeleza vita

Kupatikana miili hiyo kumeibua ukosoaji zaidi dhidi ya mpango wa Biden wa kusitisha mapigano katikati ya kampeni za urais nchini Marekani na kuongeza shinikizo dhidi ya Netanyahu kutoka kwa Waisraeli wanaomtaka kuwarejesha mateka nyumbani.

Ukosoaji huu mpya wa Biden dhidi ya Netanyahu unakuja wakati yeye na makamu wake Kamala Harris anayewania urais katika uchaguzi wa mwezi ujao pia wakikabiliwa na ongezeko la miito ya hatua kali katika kuumaliza mzozo huo uliodumu kwa miezi 11.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW