1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Biden awasili Finland kuhamasisha umoja ndani ya NATO

13 Julai 2023

Rais Joe Biden wa Marekani amewasili katika mji mkuu wa Finland, Helsinki, akikamilisha ziara yake ya wiki nzima ya kuhamasisha umoja wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO na msaada zaidi wa kijeshi kwa Ukraine.

Finnland I Gipfeltreffen amerikanisch-nordischer Staats- und Regierungschefs 2023 in Helsinki
Picha: Emmi Korhonen/Lehtikuva/REUTERS

Biden atashiriki katika mkutano wa kilele kati ya Marekani na mataifa ya Nordic yanayozijumuisha Finland, Sweden, Denmark, Iceland na Norway.

Kabla ya kurejea Washington, Biden atafanya mazungumzo na Rais Sauli Niinisto wa Finland ambaye nchi yake ndiyo imekuwa ya hivi karibuni kujiunga na NATO.

Soma zaidi: Biden afanya mazungumzo na viongozi wa Uingereza

Sweden inatarajia pia kujiunga na muungano huo wa kijeshi baada ya Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki kuondoa hivi majuzi pingamizi yake kwa taifa hilo.

Hata hivyo, uamuzi huo utatakiwa kuidhinishwa na bunge la Ankara. 

Uvamizi wa Urusi dhidi ya Ukraine umepelekea mataifa hayo ya Nordic kubadili misimamo yao ya kijeshi kwa lengo la kujilinda na uvamizi wa Moscow.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW