1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Bilawal Bhutto ateuliwa waziri wa mambo ya kigeni Pakistan

27 Aprili 2022

Waziri Mkuu mpya wa Pakistan Shehbaz Sharif amemteua Bilawal Bhutto-Zardari kuwa waziri wa mambo ya kigeni wa Pakistan. Bilawal ni mtoto wa waziri mkuu wa zamani wa taifa hilo aliyeuwawa Benazir Bhutto.

Pakistan l  Bilawal Bhutto Zardari wurde zum Außenminister ernannt
Picha: Farooq Naeem/AFP

Zardar mwenye umri wa miaka 33 na kiongozi wa chama cha PPP ni mshirika muhimu katika serikali ya mseto ya waziri mkuu Shehbaz iliyoingia madarakani hivi karibuni baada ya kuondolewa kwa utawala wa Imran Khan.

Mwanasiasa huyo kijana kutoka familia ya Bhutto yenye historia pana na siasa za Pakistan atakuwa na dhima ya kurekebisha mahusiano yaliyolegalega kati ya taifa hilo na nchi za magharibi hususani Marekani.

Baada ya kuapishwa Zardar anatarajiwa hii leo kusafiri pamoja na waziri mkuu kwa ziara nchini Saudi Arabia inayolenga kuchochea biashara na uwekezaji.
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW