1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIsrael

Blinken akutana na Abbas mjini Amman

Josephat Charo
13 Oktoba 2023

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Anthony Blinken amekutana na rais wa mamlaka ya ndani ya Wapalestina Mahmoud Abbas mjini Amman nchini Jordan.

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken akutana na Mahmoud Abbas
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken akutana na Mahmoud AbbasPicha: Jacquelyn Martin/AP Photo/picture alliance

Blinken pia amekutana na Mfalme Abdullah wa pili wa Jordan, ambaye ametahadharisha juu ya kuwahamisha Wapalestina huku Israel ikiandaa harakati kubwa ya kijeshi katika Ukanda wa Gaza.

Mfalme Abdullah wa pili amesema mzozo huo hautakiwi kuenea katika nchi jirani na kuzidisha tatizo la wakimbizi.

Blinken aliwasili Jordan jana jioni akitokea Israel na atakwenda pia Qatar, Saudi Arabia, Misri na Umoja wa Falme za kiarabu wakati Marekani ikipania kuongeza shinikizo dhidi ya kundi la Hamas.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW