1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Blinken anarejea tena Mashariki ya Kati kutafuta amani

10 Juni 2024

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken anaelekea tena Mashariki ya Kati kushinikiza mpango wa amani lakini hali ya kisiasa ya Israel na ukimya kutoka kwa kundi la Hamas unazusha swali la iwapo ataweza kufaulu.

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken akihudhuria mkutano na waandishi wa habari pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine kufuatia mazungumzo yao mjini Kyiv Mei 15, 2024.Picha: Brendan Smialowski/REUTERS

Mwanadiplomasia huyo wa juu wa Marekani, anafanya ziara yake ya nane katika eneo hilo tangu vita vilipozuka, akitarajiwa kuanza safari hiyo nchini Misri na baadae leo hii kadhalika kuelekea Israel.

Amepangiwa kufanya mazungumzo ya ndani, kwanza mjini Cairo na Rais Abdel Fattah al-Sisi, mshirika mkuu wa Marekani katika juhudi za amani na baadae mjini Jerusalem na Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu.

Blinken amepanga ziara hiyo ili kulitolea msukumo zaidi pendekezo hilo lilitangazwa Mei 31 na Rais Joe Biden ambaye ameongeza juhudi za kumaliza vita ambavyo vimewaathiri vibaya raia na kumvuruga kisiasa kabla ya uchaguzi wa Novemba wa Marekani.

Ruka sehemu inayofuata Gundua zaidi
Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW