1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaRwanda

Blinken azungumza na rais Kagame

6 Desemba 2022

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken ametowa mwito kwa rais wa Rwanda Paul Kagame kusitisha uungaji mkono anaodaiwa kuutowa kwa waasi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Ruanda | Besuch US-Außenminister Antony Blinken
Picha: Andrew Harnik/AFP/Getty Images

Hayo yametangazwa na wizara ya mambo ya nje ya Marekani jana Jumatatu ambayo pia ilisema Blinken alizungumzia wasiwasi wake kuhusu kuongezeka kwa umwagaji damu.

Msemaji wa wizara hiyo Ned Price ameeleza kwamba Blinken alizungumza kwa njia ya simu Jumapili na kiongozi huyo wa Rwanda na kuweka wazi kwamba hatua yoyote ya nje ya kuyaunga mkono makundi ya waasi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo inapaswa kusitishwa, ikiwemo uungaji mkono kutoka Rwanda kwa kundi la M23.

Blinken pia amelaani kuzuka tena kwa matamshi ya chuki na kauli za uchochezi zinazotolewa hadharani zikiilenga Rwanda na kukumbusha athari za kutisha za kauli kama hizo, zilizoshuhudiwa mwaka 1994 katika vita vya kimbari vilivyowalenga watu jamii ya kabila la Watutsi. 

Kadhalika mwanadiplomasia huyo wa ngazi ya juu wa Marekani amezitolea mwito Kongo na Rwanda kuheshimu makubaliano ya kusitisha vita yaliyofikiwa mwezi uliopita nchini Angola.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW