1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BOGOTA: Waasi waachilia watalii wa kigeni

23 Desemba 2003
Waasi wa Colombia wameaachilia huru watalii 5 wa kigeni waliokuwa wametekwa nyara miezi 2 iliopita. Watu hao ni Waisraili 4 na raia mmoja wa kingereza ambao walikuwa miongoni mwa wageni 8 waliokamatwa na waasi wa mrengo wa kushoto karibu na milima ya Sierra Nevada. 2 kati yao ambao ni Mjerumani na Muhispania waliaachiliwa huru mwezi uliopita. Mwengine wa nane ambaye ni Mwingereza alifaulu kutoroka muda mfupi baada ya kutekwa nyara na waasi hao wa Colombia.
Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW