1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaPeru

Boluarte:Bunge idhinisheni uchaguzi wa mapema

30 Januari 2023

Rais wa Peru Dina Boluarte ametoa wito kwa mara nyingine kwa bunge la nchi hiyo kuidhinisha pendekezo la kufanyika uchaguzi wa mapema kama njia ya kumaliza maandamano ya wiki kadhaa yaliosababisha vifo

Peru | Präsidentin Dina Boluarte
Picha: Angela Ponce/REUTERS

Kupitia hotuba aliyoitoa usiku wa kuamkia leo, kiongozi huyo amesemabunge linapaswa kuridhia uchaguzi mkuu ufanyike mwishoni mwa mwaka huu badala ya tarehe ya sasa ya April mwaka 2024.

 Wabunge wa nchi hiyo wanakutana kwa mara nyingine leo kujadili pendekezo hilo la serikali baada ya kulikataa siku ya Jumamosi.

Soma pia:Wabunge wa Peru wawasilisha ombi la kumng'oa rais Boluarte

 Rais Boluarte amesema iwapo wabunge watashindwa kutoa idhini ya kufanyika kwa uchaguzi mnamo mwezi Disemba atalazimika kupendekeza marekebisho ya katiba kushinikiza mpango huo.

 Hadi sasa watu 48 wameuwawa tangu Peru ilipotumbukia kwenye mzozo wa kisiasa uliochochewa na kuondolewa madarakanimwaka jana kwa rais wa wakati huo Pedro Castillo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW