1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BOMU LAUA 5 ANGOLA

16 Desemba 2003

LUANDA: Watu 5 wamefariki ndani ya trekta moja na ndani ya traila pale bomu lililozikwa ardhini liliporipuka huko Angola ya Kati. Watu 3 waliofariki papo hapo na wengine 2 wakafa baadae hospitali.Magari hayo ambayo yalitolewa zawadi na jumuiya isio ya kiserikali ya Marekani-CARE INTERNATIONAL yaliteketea. Kiasi cha mabomu ya ardhini milioni 15 yalizikwa wakati wa vita vya kienyeji nchini Angola ambavyo vilimalizika mwaka jana.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW