Bondia Mayweather kurejea ulingoni?
10 Mei 2016Matangazo
Kukiwa na ripoti hivi karibuni zinazodai kwamba wapiganaji hao wawili wanaogonga vichwa vya habari wanajadili pambano hilo, Mayweather ameuchochea uvumi huo pembezoni mwa pambano la Canelo Alvarez na Amir Khan mjini Las Vegas mwishoni mwa juma.
Mpiganaji huyo raia wa Marekani mwenye umri wa miaka 39 alistaafu Septemba mwaka jana baada ya kupata ushindi mara 49 katika kipindi cha miaka 19 ya kupigana ngumu ambapo alipata mataji ya dunia katika viwango vitano vya uzito na kujipatia kiasi cha dola milioni 800.
Mwandishi: Sekione Kitojo / rtre / afpe / dpae
Mhariri: Iddi sessanga