1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Botswana yaipatia Zimbabwe dola milioni 600

Sekione Kitojo Yusuf Saumu
27 Februari 2019

Botswana imesema itaipatia Zimbabwe karibu dola milioni 600 kuisaidia kupunguza mzozo wake wa kiuchumi.

Afrika Zimbabwe Menschenschlange vor Geldautomat
Picha: Getty Images/AFP/J. Njikizana

Botswana ambayo ina utajiri mkubwa wa madini ya Almasi imesema itaipatia Zimbabwe karibu dola milioni 600 kuisaidia nchi hiyo  kupunguza mzozo wake wa kiuchumi, gazeti la serikali la Zimbabwe The Herald limeripoti.

Mkopo  huo utatolewa  katika  sekta  ya  binafsi  nchini Zimbabwe  pamoja  na  sekta  ya  machimbo  ya  almasi, ripoti  hiyo  imesema. Waziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa Zimbabwe  James Manzou , amefichua  pendekezo  hilo kabla  ya  ziara  mjini  Harare  itakayofanywa  na  rais  wa Botswana  Mokgweetsi  Masisi.

Zimbabwe  ilitumbukia  katika  hali  mbaya  ya  kiuchumi katika  miaka  37 ya  utawala  wa  rais  Robert Mugabe ambaye  alilazimishwa  kuondoka  madarakani mwaka 2017.

Waziri  wa mambo  ya  kigeni  wa  Zimbabwe  amesema nchi  yake  inakaribisha  pendeekezo  hilo  la  Botswana  na kwamba  mkopo  huo  utasaidia  ufufuaji  wa  uchumi  wa nchi  hiyo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW