BRUSSELS: Mwito kwa Waisraeli na Wapalestina kukomesha mapambano
5 Novemba 2006Matangazo
Umoja wa Ulaya umesema unasikitishwa na hasara ya maisha ya raia wasio na hatia katika Ukanda wa Gaza na umewahimiza Waisraeli na Wapalestina kukomesha mapambano.Zaidi ya watu 40 wameuawa katika mashambulio ya siku nne yaliofanywa na vikosi vya Israel ndani na ukingoni mwa mji wa Beit Hanoun katika Ukanda wa Gaza.Rais Mahmoud Abbas wa Wapalestina,ametoa mwito kwa Umoja wa Mataifa kuingilia kati kuzuia mashambulio ya Israel.