BRUSSELS: Umoja wa Ulaya na syria zimeafikiana juu ya mapatano ya ushirikiano.
10 Desemba 2003Matangazo
Hii inafuatia miaka 5 ya majadiliano.Mjumbe wa UU Christian Leffler amewaambia maripota mjini Damscus kwamba mapatano hayo yatahusika na sekta mbali mbali pamoja na biashara,maendeleo ya jamii na ushirikiano wa kisiasa.Mapatano hayo ya ushirikiano yangali yanabidi kuidhinishwa na serikali za pande zote mbili.