1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIsrael

Bunge Israel kupigia kura leo mageuzi yanayoleta mgawanyiko

24 Julai 2023

Wabunge nchini Israel wanajiandaa leo kukipigia kura ya mwisho kipengele kikuu cha serikali ya msimamo mkali wa mrengo wa kulia kuhusu marekebisho yenye utata ya mfumo wa mahakama.

Israel | Proteste gegen Justizreform
Picha: Ilia Yefimovich/dpa/picture alliance

Hii ni hata baada ya Rais wa Marekani Joe Biden kuhimiza kuahirishwa kwa mswaada huo uliosababisha mgawanyiko na miezi kadhaa ya maandamano ya umma.

Wabunge walijadili usiku kucha wakati kukiwa na juhudi za mwisho mwisho za Rais Isaac Herzog kufikia maelewano.

Alikutana na Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu katika hospitali alikofanyiwa upasuaji wa moyo.

Netanyahu aliruhusiwa kuondoka hospitali leo na tayari yuko bungeni kwa ajili ya mchakato wa upigaji kura.

Soma pia:Maelfu waandamana kupinga mageuzi ya mahakama nchini Israel

Polisi leo wametumia mizinga ya maji ya kuwasha kuwatawanya waandamanaji waliofunga lango la bunge.

Wakosoaji wanahofia kuwa mabadiliko ya mfumo wa mahakama yatadhoofisha demokrasia ya Israel.

Sheria hiyo inayopendekezwa itaupunguza uwezo wa majaji kuyakataa maamuzi ya serikali wanayoyaona kuwa hayafai.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW