1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUfaransa

Bunge jipya ya Ufaransa kukutana Alhamisi wiki hii

15 Julai 2024

Wabunge kadhaa wa chama cha muungano wa mrengo wa kushoto nchini Ufaransa wamesema,kwamba chama hicho kinalenga kunyakuwa nafasi ya spika wa bunge wakati bunge hilo litakapofunguliwa kwa mara ya kwanza alhamisi wiki hii.

Ufaransa  | Muungano wa vyama vya mrengo wa shoto
Muungano wa vyama vya mrengo wa shoto nchini Ufaransa.Picha: Frederick Florin/AFP/Getty Images

Chama hicho kimesema kinataka kupata nafasi hiyo ili kuwa na nguvu bungeni licha ya kutokuwa na wingi mkubwa wa viti na kinashindwa  kuunda serikali baada ya uchaguzi wa mapema wa bunge.

Wabunge watakuwa na jukumu Alhamisi la kumchaguwa spika,ambayo ni nafasi muhimu katika kipindi hiki ambacho rais Emmanuel Macron amedhoofika kisiasa na bunge likiwa na mgawanyiko kutoka na kutokuwepo chama au kundi lenye wingi wa kutosha wa kudhibiti mamlaka peke yake.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW