Bunge la Ulaya laalani hatua ya kushikiliwa Tundu Lissu
8 Mei 2025
Matangazo
Katika azimio lao, wabunge wa Ulaya wamelaani kukamatwa kwa kiongozi huyo na kueleza wasiwasi wao mkubwa kuhusiana na tuhuma za kisiasa dhidi yake ambazo hukumu yake huenda ikawa ni kifo.
Aidha Bunge hilo la Ulaya limezitaka mamlaka za Tanzania kurejesha ushiriki kamili wa Chadema katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025, kufanya mazungumzo na vyama vyote vya siasa kuhusu mageuzi ya uchaguzi, kuheshimu haki za vyama vya siasa na kuhakikisha uchaguzi huru na wa haki.