1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Bunge la Ulaya lapitisha sheria kuhusu uhamiaji

26 Machi 2026

Bunge la Ulaya limeidhinisha leo sheria mpya zinazolenga kuharakisha mchakato wa kuwahamisha waomba hifadhi ambao maombi yao yamekatiliwa ikiwa ni pamoja na kuanzisha vituo vya wahamiaji nje ya mipaka ya Umoja wa Ulaya.

Ubelgiji Brussels 2026 | Bunge la Ulaya
Kikao cha bunge la Ulaya mnamo Januari 7, 2026Picha: Virginia Mayo/AP Photo/picture alliance

Kura hiyo ya leo inaruhusu wabunge wa Umoja wa Ulaya kuingia katika mazungumzo na nchi wanachama ili kukamilisha sheria hiyo ya uhamiaji.

Maamuzi hayo tata, yaliungwa mkono na wabunge 389 wa Umoja huo, huku 206 wakiyapinga na 32 wakijizuia kupiga kura.

Iwapo itaidhinishwa, sheria hiyo huenda ikawezesha kuanzishwa kwa vituo vya kuwapokea wahamiaji waliokataliwa nje ya Umoja huo wa Ulaya.

Marekebisho hayo pia yanalenga kuwapa fursa waomba hifadhi waliokataliwa kuondoka katika Umoja huo kwa hiari.

Chini ya sheria hiyo, waomba hifadhi waliokataliwa watalazimika kushirikiana katika kurejeshwa makwao.

Wahamiaji watakaokataa kufanya hivyo wanaweza kukabiliwa na adhabu, ikiwa ni pamoja na kupunguzwa kwa msaada kwao ama pia kupokonywa hati zao za kusafiria.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW