1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Burhan asema vita havitokwisha Sudan hadi RSF wasalimu amri

30 Machi 2025

Kiongozi wa kijeshi nchini Sudan Abdel Fattah al-Burhan ameapa kwamba wanajeshi wake wataendelea na mapambano dhidi ya kundi la wanamgambo wa RSF, hadi kundi hilo litakapoweka chini silaha zake.

Abdel Fattah al-Burhan
Kiongozi wa kijeshi nchini Sudan Abdel Fattah al-Burhan Picha: Sudan Transitional Sovereignty Council/Handout via REUTERS

Katika hotuba yake ya kwanza tangu jeshi lake lilipochukua udhibiti wa mji Mkuu Khartoum, Al Burhan amesema mwisho wa vita vya takriban miaka miwili kati ya pande hizo mbili hasimu utawezekana tu iwapo kundi hilo litaweka chini silaha zake. 

Kiongozi huyo wa kijeshi ameondoa uwekekano wa mazungumzo kati ya pande hizo mbili akiapa kupambana nao hadi mwisho.

"Kwa watu wa Sudan, njia ya amani na kumaliza vita bado iko wazi. Kuteseka kwa watu wetu katika maeneo yanayoshikiliwa na wanamgambo, kuzingirwa kwao, kuuwawa na uharibifu hasa katika eneo la El Fasher, na umuhimu wa kueneza amani na uthabiti katika nchi hii...Haya yote yanawezekana na njia iko wazi. ni lazima wanamgambo waweke chini silaha zao," alisema al Burhan.

Jeshi la Sudan lasema limerejesha udhibiti wa mji mkuu

Hotuba ya Burhan imekuja siku kadhaa kuidhibiti Ikulu ya rais iliyokuwa chini ya RSF tangua kuanza kwa vita hivyo takrioban miaka miwili iliyopita. Hata hivyo kiongozi wa wanamgambo hao Mohammed Hamdan Dagalo amesema kamwe hawatosalimu amri.