1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaBurundi

Burundi yamchagua mpatanishi wa kitaifa

17 Novemba 2022

Bunge nchini Burundi limemchaguwa Bi Aimée Lorentine Kanyana kuwa mpatanishi wa kitaifa. Jumla ya wabunge 120 walioshiriki uchaguzi huo

Burundi Bujumbura | Evariste Ndayishimiye, Präsident
Picha: Bujumbura Amida Issa/DW

Bunge nchini Burundi limemchaguwa Bi Aimée Lorentine Kanyana kuwa mpatanishi wa kitaifa. Jumla ya wabunge 120 walioshiriki uchaguzi huo, 109 wamepiga kura kuchaguwa mmoja kati ya wagombea 13 wa nafasi hiyo ya mpatanishi wa Warundi. Aimée Lorentine Kanyana, aliyewahi kuwa waziri wa sheria wa Burundi, ni mtu wa tatu kushikilia nafasi hiyo, baada ya Hayati Mohammed Rukara na Édouard  Nduwimana ambaye muhula  wake umefikia ukingoni. Taasisi ya mpatanishi wa kitaifa ilianzishwa na Mkataba wa Amani uliosainiwa Agosti 28 mwaka 2020 jijini Arusha, Tanzania, chini ya usuluhishi wa aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini, Nelson Mandela.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW