1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Burundi yatangaza siku 7 za kumuomboleza Rais Nkurunziza

10 Juni 2020

Serikali ya Burundi imetangaza maombolezo ya kitaifa ya siku 7 kufuatia kifo cha rais wake Pierre Nkurunziza, aliyeaga dunia Jumatatu akiwa na umri wa miaka 55 kutokana na mshituko wa moyo.

Präsident Burundis Pierre Nkurunziza
Picha: Reuters/E. Ngendakumana

Tangazo la serikali kwenye Redio na Televisheni ya taifa lililosomwa na msemaji wake Prosper Ntahorwamiye ambaye pia ni Katibu mkuu wa serikali lilisema Nkurunziza alifariki dunia kutokana na mshituko wa moyo katika hospitali ya mkoani Karuzi.

Kulingana na katiba ya Burundi spika wa Bunge Pascal Nyabenda ndiye atakayeshika hatamu za uongozi kwa kipindi cha miezi miwili hadi atakapotawazwa Evariste Ndayishimiye aliyeibuka na ushindi kwenye uchaguzi wa rais wa Mei 20 mwaka huu.

Hata hivyo taarifa nyingine zinasema muhula wa bunge ulimalizika tangu April 27 ilipozinduliwa kampeni ya uchaguzi hivyo ni makamu wa rais atakayeshika hatamu.

Nkurunziza aliiongoza Burundi kwa kipindi cha miaka 15.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW