CAF: Waliozusha vurugu fainali ya AFCON kuadhibiwa
19 Januari 2026
Kupitia taarifa rasmi, CAF imesema inalaani vikali tabia isiyokubalika iliyoonyeshwa na baadhi ya wachezaji na maafisa wakati wa fainali ya jana Jumapili. Taarifa hiyo imeongeza kuwa michuano ya AFCON inapaswa kuwa mfano wa nidhamu, heshima na ushindani wa kiungwana, na kwamba vitendo vinavyokiuka maadili hayo haviwezi kuvumiliwa.
CAF imeweka msisitizo juu ya uchunguzi wa kina na kuchukua hatua dhidi ya wahusika binafsi, iwe ni wachezaji, maofisa wa benchi la ufundi au viongozi wa timu
Katika fainali hiyo iliyochezwa mjini Rabat, wachezaji wa Senegal waliondoka uwanjani kama ishara ya kupinga uamuzi wa refarii Jean-Jacques Ndala baada ya kuwapa wenyeji Morocco penalti katika dakika za mwisho za muda wa nyongeza, wakati mchezo ukiwa bado 0-0.