1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Cambodia na Thailand zaendelea kushambuliana

13 Desemba 2025

Cambodia na Thailand zimeripoti leo kuendelea kwa mashambulizi yaliolenga pia maeneo ya kiraia, licha ya Rais wa Marekani Donald Trump kusema kwamba mataifa hayo jirani yamekubaliana kusitisha mapigano.

Cambodia Preah Vihear 2025 | Wakazi wakimbia eneo
Wakazi wa eneo la mpaka la Preah kati ya Thailand na Cambodia wakimbia mapigano mnamo Desemba 8, 2025Picha: Str/AFP

Katika chapisho kwenye mtandao wa Facebook, wizara ya ulinzi ya Cambodia imesema vikosi vya Thailand bado havijasitisha mashambulizi yake.

Kwa upande wake, jeshi la Thailand liliandika kwenye X kwamba Cambodia ilirusha makombora kwenye maeneo ya kiraia katika mkoa wa Sisaket, na kuwajeruhi raia wanne.

Waziri Mkuu wa Thailand Anutin Charnvirakul, pia ameviambia vyombo vya habari vya ndani kwamba hakukuwa na usitishaji mapigano katika mzozo huo wa mipaka.

Baada ya mawasiliano na Trump, Anutin aliwaambia waandishi wa habari huko Bangkok kwamba lazima Cambodia iwe ya kwanza kusitisha mapigano.

Amesema upande uliokiuka makubaliano ya kusitisha mapigano ndio unaopaswa kurekebisha mienendo yake na wala sio ulioushambuliwa.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW