1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

CANBERRA: Siasa kuhusu wakimbizi yabadilishwa

18 Juni 2005

Australia imeregeza siasa yake iliyozusha mabishano ya kuwatia ndani moja kwa moja wakimbizi wanaoingia Australia kwa njia zisizo halali.Waziri mkuu John Howard amelazimika kubadilisha msimamo wake,baada ya wanachama wenzake katika serikali yake kutishia kuwa watakwenda upande wa upinzani,wakilalamika dhidi ya kile walichokieleza kuwa ni utaratibu usio na huruma.Badiliko kubwa lililofanywa ni kuwa familia zenye watoto,sasa zitapelekwa katika jamii badala ya kuwekwa kizuizini kwenye vituo maalum.Miongoni mwa mageuzi mengine ni kuharakisha utaratibu wa ukaguzi wa maombi ya ukimbizi.Nchini Australia,tawi la shirika la Amnesty International linalopigania haki za binadamu duniani,limefurahia mageuzi hayo,lakini kwa wakati huo huo limesisitiza kuwa bado kuna mambo yanayotia shaka.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW