CDC yathibitisha mlipuko wa Ebola nchini Kongo
15 Mei 2026
Matangazo
Taarifa hiyo imetolewa leo Ijumaa na Kituo cha Udhibiti wa Magonjwa barani Afrika, CDC, ambacho kimesema visa vya mwanzo vimeripotiwa kwenye jimbo la Ituri.
CDC imesema inafuatilia kwa karibu mlipuko huo na inasaidia utayari wa kukabiliana na kusambaa zaidi ugonjwa huo ndani ya Kongo pamoja na kwenye mataifa jirani.
Ugonjwa wa Ebola uliogunduliwa kwa mara ya kwanza mwaka 1976 hutokana na virusi vinavyosambazwa na jamii fulani ya popo walao matunda.
Ugonjwa huo ambao husababisha mgonjwa kuvuja damu na athari kwenye viungo muhimu vya mwili umewaua zaidi ya watu 15,000 barani Afrika tangu ulipogunduliwa miaka 50 iliyopita.