1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Chama cha AfD kupata mafanikio katika uchaguzi wa Ulaya

Saleh Mwanamilongo
2 Juni 2024

Kura ya maoni yaonyesha chama cha siasa kali za mrengo wa kulia cha AfD cha nchini Ujerumani kushika nafasi ya pili katika uchaguzi wa bunge la Ulaya.

Uchunguzi wa maoni uliofanywa na taasisi ya INSA, chama cha AfD huenda kikapata asilimia 16 ya kura katika uchaguzi wa bunge la Ulaya
Uchunguzi wa maoni uliofanywa na taasisi ya INSA, chama cha AfD huenda kikapata asilimia 16 ya kura katika uchaguzi wa bunge la Ulaya Picha: Müller-Stauffenberg/IMAGO

Hayo ni kwa mujibu wa kura mpya ya maoni ya taasii ya INSA. Kama uchaguzi wa Ulaya ungefanyika Jumapili ya Juni 2, chama Mbadala cha Ujerumani, AfD kingepata asilimia 16 ya kura mbele ya chama cha Social Democratic (SPD) cha Kansela Olaf Scholz.

Muungano wa kihafidhina wa Ujerumani wa vyama vya Christian Democratic Union, CDU na chama cha Christian Social Union, CSU ulioneka kushika nafasi ya kwanza kwa asilimia 29 ya kura.

Kuelekea uchaguzi huo wa bunge la Ulaya, wakuu wa viwanda na vyama vya wafanyakazi nchini Ujerumani wameonya huenda kukawa na athari kubwa kwa taifa hili pamoja na uchumi wake iwapo Chama cha AfD kitapata mafanikio katika uchaguzi huo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW