Chama cha BNP Bangladesh chadai ushindi kwa wingi bungeni
13 Februari 2026
Kupitia mtandao wa X, BNP imedai kupata viti vya kutosha kuunda serikali, ingawa chama hasimu, Jamaat-e-Islami, kilieleza wasiwasi kuhusu ucheleweshaji wa kutangaza matokeo rasmi. BNP inaongozwa na Tarique Rahman mwenye umri wa miaka 60, anayewania nafasi ya waziri mkuu, ambaye alirejea Bangladesh mwezi Desemba baada ya kuishi uhamishoni London kwa miaka 17.
Tume ya Uchaguzi bado haijatoa matokeo ya mwisho, lakini vyombo kadhaa vya habari vya ndani vimeripoti kuwa BNP imevuka idadi ya viti 151 vinavyohitajika kupata wingi wa wabunge katika Bunge lenye jumla ya viti 350, ikiwa ni pamoja na viti 50 maalumu kwa wanawake vinavyogawiwa kwa uwiano wa ushindi wa vyama.
Huu ni uchaguzi wa kwanza baada ya mapinduzi ya umma yaliyoongozwa na vijana kumng'oa madarakani Waziri Mkuu Sheikh Hasina mwaka 2024.