1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Chama cha Kabila chasema hukumu dhidi yake ni ya kisiasa

1 Oktoba 2025

Chama cha rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Joseph Kabila cha People's Party for Reconstruction and Democracy, kimesema hukumu ya kifo iliyotolewa dhidi ya Kabila imeendeshwa kisiasa na haikuwa ya haki.

Johannesburg, Afrika Kusini 2025 | Joseph Kabila, Rais wa zamani wa Kongo
Mashirika ya kutetea haki za binadamu yameonya hukumu hiyo inaweza kuongeza mgawanyikoPicha: Siphiwe Sibeko/REUTERS

Katibu Mkuu wa chama hicho, Emmanuel Ramazani Shadary amesema wanaamini ni wazi kuwa nia ya utawala wa kidikteta uliopo madarakani ni kumtenganisha Kabila na siasa.

Jana, Mahakama ya Kijeshi ilimuhukumu Kabila adhabu hiyo baada ya kukutwa na hatia ya kuliunga mkono kundi la waasi wa M23, ambalo limechukua udhibiti wa eneo la mashariki mwa Kongo.

Hata hivyo, Kabila, alihukumiwa bila ya kuwepo mahakamani.

Richard Bondo, wakili aliyeyawakilisha majimbo ya Kivu Kusini na Kaskazini amesema ameridhishwa na uamuzi wa mahakama.

Mashirika ya kutetea haki za binadamu yameonya kuwa hukumu dhii ya Kabila inaweza kuongeza mgawanyiko katika taifa hilo kubwa lenye utajiri wa madini, ambalo limekumbwa na vita na ukosefu wa utulivu kwa zaidi ya miongo mitatu.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW