1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaJapan

Chama tawala nchini Japan chamteua mwanamke kuwa Mwenyekiti

6 Oktoba 2025

Chama tawala nchini Japan cha Liberal Democratic Party (LDP) kimempata kiongozi wake mpya ambaye ni Waziri wa zamani wa Uchumi Sanae Takaichi.

Tokyo 2025 | Mwenyekiti Mpya wa chama tawala nchini Japan cha LDP Sanae Takaichi
Waziri wa zamani wa uchumi Sanae Takaichi, Mwenyekiti Mpya wa chama tawala nchini Japan cha Liberal Democratic Party (LDP) Picha: Kim Kyung-Hoon/POOL/AFP/Getty Images

Sanae Takaichi mwenye umri wa miaka 64, ni mhafidhina mwenye msimamo mkali ambaye anatarajiwa kuwa  waziri mkuu  wa kwanza mwanamke nchini humo,  atahitaji kutafuta njia za kukidumisha madarakani  chama chake cha Kiliberali na kupata tena uungwaji mkono wa umma kwa kuchukua hatua za kushughulikia tatizo la mfumuko wa bei na kukabiliana na changamoto mbalimbali za kidiplomasia.

Bi Sanae Takaichi ambaye ni mfuasi mkubwa wa maono ya kihafidhina ya Waziri Mkuu wa zamani wa  Japan  Shinzo Abe, yuko kwenye hatihati ya kupoteza ushirika wa muda mrefu wa chama cha siasa za mrengo wa kati cha Komeito kutokana na siasa zake za kihafidhina.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW