Chama tawala nchini Malawi chadai kuvurugwa kwa matokeo
20 Septemba 2025
Matangazo
Tume ya Uchaguzi ya Malawi (MEC) ilitoa matokeo yake ya kwanza jana, huku matokeo kutoka kwa mabaraza matatu ya miji kati ya manne yakionyesha ushindi mkubwa kwa Peter Mutharika, mgombea wa upinzani, mwenye umri wa miaka 85.
Lakini muda mfupi kabla ya matokeo hayo, MCP ilisema katika mkutano na waandishi wa habari kwamba wawakilishi wake wamegundua kasoro za uchaguzi katika wilaya 13 kati ya 28 za nchi hiyo.
Mgombea mwenza wa Rais Lazarus Chakwera wa chama hicho cha MCP Vitumbiko Mumba, amesema MCP imewasilisha malalamiko rasmi kwa tume ya uchaguzi kuhesabu upya kura hasa katika maeneo waliyogundua kasoro kubwa.
Wakati huo huo, polisi nchini humo imesema imewakamata makarani wanane wa data kwa madai ya kuvuruga matokeo hayo ya uchaguzi.