1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

Chanzo: Mazungumzo kati ya DRC na M23 yanaendelea "vyema"

11 Julai 2025

Mazungumzo kati ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda yanaendelea katika mwelekeo sahihi baada mkutano kufanyika mjini Doha.

Goma 2025 | Waasi wa M23 wakiwa Mashariki mwa DRC
Waasi wa M23 wakiwa mjini Goma, Mashariki mwa DRCPicha: Arlette Bashizi/REUTERS

Hayo yameelezwa na mwanadiplomasia wa Qatar kwa sharti la kutotajwa jina akisisitiza kuwa wawakilishi wa pande hizo mbili wanajadiliana kuhusu namna ya kupunguza mateso ya wakazi wa Mashariki mwa Kongo, kuimarisha mpango wa usitishaji mapigano na kuhimiza hatua zaidi kuelekea maridhiano.

Wiki iliyopita,  waasi wa M23  walishauri kufanyike mazungumzo zaidi yatakayoshughulikia matatizo ambayo hayakujadiliwa katika makubaliano ya amani kati ya Rwanda na Kongo yaliyotiwa saini mjini Washington mwezi uliopita yakilenga kumaliza mzozo wa miongo kadhaa huko mashariki mwa Kongo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW