Chapo afuta ziara yake ya Davos kutokana na mafuriko
19 Januari 2026
Matangazo
Katika chapisho kwenye mtandao wa Facebook hapo jana, Chapo amesema Msumbiji inapitia wakati mgumu na kipaumbele kwa wakati huu ni kuokoa maisha.
Mvua kubwa iliyonyesha tangu katikati ya Desemba imesababisha mafuriko makubwa
katika mikoa ya Gaza, Maputo na Sofala nchini humo, huku mabonde ya mito yakiongeza maji yake kufikia viwango vya kutisha.
Haya ni kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa jana na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Uratibu wa Masuala ya Kibinadamu, OCHA.
OCHA imesema mamlaka imekadiria kuwa zaidi ya watu 400,000 wameathirika, huku idadi hiyo ikitarajiwa kuongezeka katika wakati ambapo mvua inaendelea kunyesha.
Mvua kubwa pia imeathiri maeneo ya Afrika Kusini, ikiwa ni pamoja na kaskazini mashariki ilipo mbuga yake ya kitaifa ya Kruger .