1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaChina

China imesitisha mazungumzo ya kudhibiti silaha na Marekani

18 Julai 2024

China imetangaza kusitisha mazungumzo ya udhibiti wa silaha na Marekani, ikiwa ni hatua ya kupinga kitendo cha Marekani kufanya biashara ya silaha na Taiwan.

China | Lin Jian
Lin Jian, Msemaji mpya wa Wizara ya Mambo ya Nje akizungumza wakati wa Mkutano wa Kawaida wa Wanahabari Machi 22, 2024.Picha: Ichiro Ohara/Yomiuri Shimbun/AP Photo/picture alliance

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China, Lin Jian amesema kitendo cha hivi karibuni cha Marekani kurudia kuiuzia Taiwan silaha kunahatarisha mazingira ya kisiasa kwa ajili ya kuendelea na mashauriano ya kudhibiti silaha.

Lin alisema China iko tayari kudumisha mawasiliano katika udhibiti wa silaha za kimataifa, lakini Marekani lazima iheshimu misingi ya China na kujenga mazingira muhimu kwa ajili ya majadiliano.

Maafisa wa Marekani na  China walianzisha tena majadiliano kuhusu silaha za nyuklia mwezi Novemba, lakini mazungumzo rasmi ya kudhibiti silaha hayakutarajiwa kufanyika hivi karibuni katikati ya wasiwasi wa Marekani kuhusu China kuharakisha katika kutengeneza silaha za nyuklia.

China inadai kisiwa hicho chenye mamlaka yake ya kidemokrasia ni himaya yake.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW