1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

China na Marekani zatakiwa kupunguza mvutano wa kibiashara

23 Aprili 2020

Wizara ya Biashara ya China imesema China na Marekani zinapaswa kutumia awamu ya kwanza ya makubaliano ya biashara kati yao kama fursa ya kujitahidi kupunguza masuala yanayosababisha mashaka ya kibniashara kati yao.

US-Präsident Donald Trump (R) und der chinesische Präsident Xi Jinping in der Großen Halle des Volkes in Peking
Picha: picture-alliance/dpa

Wizara hiyo pia imeyataka mataifa yote mawili kuepuka kuwekeana vikwazo vipya vya biashara na uwekezaji. Msemaji wa wizara hiyo ya ya Biashara ya China Gao Feng, ameuambia mkutano wa habari kuwa mataifa hayo mawili yanapaswa kujongeleana, kuongeza ushirikiano na kusimamia tofauti zao.

Amesema hatua hizo ni muhimu katika kufufua uchumi wa dunia ulioathiriwa vibaya na mzozo wa janga la virusi vya corona.

China inapanga kununua zaidi tani milioni 30 za mazao ya kilimo kuisaidia kujilinda dhidi ya vurugu zilizotokea katika mfumo wa ugavi kutokana na janga la corona, na pia kutimiza ahadi ya kununua mazao zaidi kutoka Marekani.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW