1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

China, Ujerumani kuzingatia uwazi na ushindani wa haki

25 Februari 2026

China na Ujerumani zimesisitiza umuhimu wa majadiliano yanayozingatia uwazi, ushindani wa haki na kuhakikisha upatikanaji wa masoko wenye usawa kati ya pande hizo mbili.

China, Peking 2026
Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz na Rais wa China, Xi JinpingPicha: Michael Kappeler/dpa/picture alliance

Hayo ni kulingana na kauli ya pamoja iliyotolewa na Rais wa China Xi JinPing pamoja na Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz aliye ziarani Beijing.

Kando ya hayo mataifa hayo yamesema yanaunga mkono juhudi za kupata makubaliano ya kusitisha vita na amani ya kudumu nchini Ukraine kwa kuzingatia mkataba wa Umoja wa Mataifa.

Mabadiliko ya tabia nchi kuzingatiwa

China na Ujerumani zimekubaliana pia kuendeleza mazungumzo kuhusu mabadiliko ya tabianchi.  Katika hatua nyingine baada na mazungumzo yake na Rais Xi, Kansela wa Ujerumani amesema China itanunua takriban ndege 120 kutoka kwa kampuni kubwa ya usafiri wa anga ya Ulaya ya Airbus.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW