China yaapa kulinda ulinzi wa pamoja wa kiusalama na Urusi
3 Novemba 2025
Matangazo
Aliyasema hayo wakati wa ziara ya Waziri Mkuu wa Urusi nchini humo Mikhail Mishustin. Katika mazungumzo yao yaliyofanyika mjini Hangzhou, Li amesema Urusi na China ni marafiki na washirika wazuri wanaoaminiana.
Mishustin yupo katika ziara ya siku mbili China ambako shirika la habari la taifa TASS limesema hapo kesho waziri mkuu huyo atakuwa na mazungumzo na rais Xi Jinping.
Mazungumzo yao yanatarajiwa kutuwama katika masuala ya Uchumi na ushirikiano wa teknolojia, wakati Urusi ikijaribu kukabiliana na vikwazo vya Magharibi kufuatia vita vyake Ukraine na China nayo ikivutana na Marekani kuhusu masuala ya kibiashara na kiteknolojia.