1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

China yaimarisha ulinzi dhidi ya janga la virusi vya Corona

Sekione Kitojo
26 Januari 2020

China leo Jumapili(26.01.2020) imeongeza hatua zake za vizuwizi vya kusafiri kujaribu kuudhibiti ugonjwa unaosababishwa na virusi vya corona ambao umekwishawauwa watu 56 na wengine 2,000 wameambukizwa.

China Wuhan Hygienemaßnahmen wegen Coronavirus
Picha: picture-alliance/AP Photo

 

Wakati huo huo Marekani, Ufaransa na  Japan zinajitayarisha kuwaondoa  raia wao kutoka katika  mji ulioko katika karantini ambao ndio chimbuko la virusi hivyo wa Wuhan.

Mfanyakazi wa hospitali (kushoto) akivalia kizuwizi puani,akimpima mtu iwapo ana homa itokanayo na virusi vya CoronaPicha: Getty Images/AFP/H. Retamal

China imezuwia watu kuingia  ama kutoka  kutoka  katika  mji ulioathirika  zaidi katika  jimbo  la  Hubei katikati ya  nchi hiyo katika operesheni kamambe inayowaathiri  mamia  kwa  mamilioni  ya  watu ili  kuweza  kupunguza  kasi ya  ugonjwa  huo unaoathiri njia ya kupumua.

Uwezo wa  virusi hivyo kusambaa  "unaonekana kuwa imara  zaidi , licha  ya  kuwa , si vyenye nguvu  sana  kama  virusi vya  SARS", maafisa wa  afya  wa  ngazi ya juu  nchini  China  wamesema  katika mkutano na  waandishi  habari, na  kuongeza  kuwa  uelewa  wao kuhusu virusi  hivyo una mipaka.

Virusi  vya  hapo  kabla  visivyojulikana  vilisababisha  wasi wasi mkubwa  duniani  kwasababu ya  ukaribu  wake  kama  virusi vya SARS, virusi vilivyosababisha matatizo makubwa ya kupumua, ambavyo vimeuwa  mamia  ya  watu  nchini  China na  Hong Kong mwaka 2002-2003.

Nje ya  eneo ulipoanzia ugonjwa huo, miji minne, ikiwa ni  pamoja beijing  na  Shanghai, na  jimbo  la mashariki la Shandong, imetangaza  marufuku kwa  mabasi yanayosafirisha  abiria  masafa marefu kuingia ama  kutoka  katika  mipaka yake, hatua  ambayo itawaathiri mamilioni  ya  watu  wanaosafiri  kwa  ajili  ya sikukuu  ya mwaka mpya.

China inajenga haraka hospitali itakayochukua wagonjwa 1,000 mjini Wuhan kwa azma ya kupambana na virusi vya CoronaPicha: picture-alliance/dpa/AP/Chinatopix

Wakaazi kuvaa vizuwizi usoni

Jimbo  maarufu  la  mashariki la Guandong, Jiangxi katikati ya nchi hiyo, na  miji mitatu imeweka  ulazima kwa wakaazi  kuvaa vifunika uso wakiwa katika  maeneo ya watu wengi.

Ukianzia  katika  mji mkuu wa jimbo  la  Wuhan , Hubei, virusi  hivyo vilisambaa  nchini  China na  duniani , ambapo maambukizi yalithibitishwa  katika  karibu nchi 12 hadi Marekani.

Wizara ya mambo ya  kigeni  ya  Marekani imesema  leo Jumapili (26.01.2020) kuwa inapanga safari ya ndege kutoka  Wuhan kwenda  San Francisco kwa wafanyakazi wake wa  ubalozi mdogo pamoja  na  Wamarekani wengine katika  mji huo.

Safari hiyo ya ndege siku ya  Jumanne, imesema  katika  taarifa  ya barua  pepe kwa  Wamarekani wote  nchini China  ambayo inaonya, uwezo mdogo sana kwa kuwachukua raia  wa  kawaida.

Wananchi mjini Beijing wakivalia vitambaa vya kufunika mdomo na pua kuzuwia kusambaa kwa virusi vya coronaPicha: picture-alliance/newscom/UPI PHoto/S. Shaver

Serikali ya  Ufaransa na  kampuni ya  Ufaransa  ya  kuunda  magari ya  PSA pia imesema  wanatayarisha  mipango  kuwaondoa wafanyakazi  na  famiali  zao , ambao  wanawekwa  katika  karantini katika  mji uliopo katika  jimbo  jirani.

Japan inafanya uratibu na  serikali  ya  China kuwaondoa  haraka raia  wake, waziri mkuu Shinzo Abe  amesema.

Ubalozi mdogo  wa  Korea  kusini mjini  Wuhan umesema  unafanya taratibu  za  kuwahesabu raia wake kupitia  mtandaoni  ili  kujua mahitaji ya  ndege za kukodi zinazohitajika.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW