1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

China yakumbwa na mashambulizi ya mtandaoni

23 Septemba 2024

Wizara ya usalama wa taifa ya China imesema kumekuwa na mashambulizi ya mtandaoni yanayofanywa na kundi la wadukuzi lijiitalo Anonymous 64 kwenye maeneo ya China Bara, Hong Kong na Macau.

Alama ya mashambulizi ya mtandaoni.
Alama ya mashambulizi ya mtandaoni.Picha: Pond5 Images/IMAGO

Kwa mujibu wa wizara hiyo iliyotolewa leo, mashambulizi hayo yanasambaza ujumbe unaokashifu viongozi na mfumo wa kisiasa wa China Bara na sera za kimsingi za taifa hilo la kikomunisti.

Wizara hiyo imewataka raia kuripoti matukio yoyote yanayojiri kwenye vifaa vyao ya kieletroniki kuhusiana na mashambulizi hayo.

Soma zaidi: Waziri wa Ulinzi China ahimiza mataifa makubwa kuongoza juhudi za amani duniani

Mara kadhaa, watumiaji wa simu za mkononi, kompyuta ama televisheni hutumiwa ujumbe kwenye vifaa vyao wenye picha na maelezo ya kumlaani Rais Xi Jinping.

China inaamini kuwa kundi hilo la wadukuzi lina makao yake nchini Taiwan.

Taiwan yenyewe imekuwa ikisema kuwa makundi ya wadukuzi wa China yamekuwa yakisambaza taarifa za uongo kwenye kisiwa hicho kinachojitawala chenyewe.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW