1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaChina

China yasema msimamo wake haujabadilika kuhusu Rasi ya Korea

20 Februari 2023

China imesema ina wasiwasi kuhusu hali inayoendelea katika Rasi ya Korea.

Karte Krise Nordkorea Südkorea Yeonpyeong Inseln Flash-Galerie

Kauli hiyo imetolewa leo na msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China, Wang Wenbin, baada ya Korea Kaskazini kurusha makombora ya masafa mafupi mapema leo asubuhi.

Korea Kaskazini imefyatua makombora mawili katika pwani yake ya mashariki, huku Kim Yo Jong, dada wa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un, mwenye nguvu na ushawishi mkubwa, akisema kuwa hatua ya Korea Kaskazini kuitumia Bahari ya Pasifiki kama eneo lake la kufyatua makombora, itategemea tabia ya vikosi vya Marekani.

Wakati huo huo, Japan imetoa ombi la kufanyika mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa baada ya Korea Kaskazini kufyatua makombora hayo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW