1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Comoro yaweka marufuku ya kutotoka nje usiku

18 Januari 2024

Wizara ya mambo ya ndani ya Comoro imeweka marufuku ya kutoka nje usiku katika taifa hilo lililo katika Bahari ya Hindi baada ya kuzuka kwa maandamano ya kupinga kuchaguliwa kwa mara nyengine kwa Rais Azali Assoumani.

Azali Assoumani
Rais wa Comoro Rais Azali Assoumani.Picha: Ludovic Marin/AFP/Getty Images

Hapo jana jeshi lilifyatua mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji katika Mji Mkuu Moroni ila mapema leo bado waandamanaji walionekana kaskazini mwa mji huo.

Msemaji wa serikali ya Comoro Houmed Msaidie amewalaumu wafuasi wa wagombea wa upinzani walioshindwa uchaguzi kwa maandamano hayo.  Msaidie amesema waandamanaji kadhaa wamekamatwa.

Wasiwasi watanda visiwani Comoro baada ya Azali Assoumani kutangazwa mshindi katika uchaguzi wa rais

Assoumani ameiongoza Comoro tangu kuingia madarakani kupitia mapinduzi mwaka 1999.

Kulingana na tume ya kitaifa ya uchaguzi, alipata asilimia 62.97 ya kura katika uchaguzi uliopita.