1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

CONMEBOL yachukizwa na uamuzi wa FIFA

Josephat Charo
9 Mei 2020

Uamuzi wa FIFA kuruhusu wachezaji watano wa akiba katika kila mechi kusaidia kukabiliana na msongamano wa ratiba za mechi umepokewa kwa mshangao Amerika ya Kusini siku ya Ijumaa (08.05.2020)

Kolumbien 2019 | Copa América | Alejandro Dominguez, Präsident CONMEBOL
Picha: Getty Images/G. Legaria

"Mabadiliko haya yametushangaza, hayakufanywa kwa mashauriano na shirikisho letu," Alejandro Dominguez (pichani) rais wa Shirikisho la soka la Amerika Kusini, CONMEBOL, aliandika katika mtandao wa kijamii wa twitter.

Mapema Ijumaa shirikisho la soka ulimwenguni FIFA liliziruhusu timu kuwa na wachezaji watano wa akiba kila mechi, badala ya watatu kama ilivyo kawaida, kama hatua ya muda kusaidia kukabiliana na msongamano wa ratiba za mechi huku mechi zikirejea baada ya kusitishwa kutokana na janga la virusi vya corona.

Mabadiliko hayo katika sheria yataruhusiwa katika mashindano yote yatakayokamilika mwishoni mwa mwaka 2020 na litakuwa jukumu la waandaaji wa mashindano hayo kuamua kuyatekeleza, ilisema FIFA.

Dominguez alisema shirikisho la CONMEBOL litaitisha kikao maalumu cha wataalamu kuuchambua uamuzi huo na kuamua kama unafaa kutumika katika mashindano ya Amerika Kusini kama vile Copa Libertadores.

(reuters)

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW