1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

CR atunukiwa Njumu ya Dhahabu

14 Oktoba 2015

Mchezaji nyota wa Ureno Cristiano Ronaldo ametunukiwa kiatu cha Dhahabu kwa Ufungaji Bora barani Ulaya na kuweka rekodi kwa kutwaa taji hilo kwa mara ya nne

Portugal Cristiano Ronaldo und Jorge Mendes
Picha: picture-alliance/epa/J. Montero

Katika msimu wa 2014/15, Ronaldo alifunga mabao 48 kwenye ligi kuu ya Uhispania La Liga na kutwaa Njumu ya Dhahabu kwa mara 3 akiwa na miamba Real Madrid

Msimu wa 2007/08 akiwa na Manchester United alitwaa tena kiatu hicho baada ya kuwa mfungaji bora. Hii ni mara ya kwanza katika Historia ya Miaka 47 ya Tuzo hii ya Njumu ya Dhahabu kwa Mfungaji Bora wa Ligi za Ulaya kuichukua mara 4.

Ronaldo, ameifungia Real Madrid jumla ya mabao 323, na kufikia rekodi ya mabao mengi iliyokua imewekwa na mchezaji wa zamani wa timu hiyo Raúl González aliyefungia timu hiyo mabao 323.

Mwandishi: Bruce Amani/AFP
Mhariri: Abdulrahman

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW