Asili na mazingiraUmoja wa Falme za Kiarabu
Dhahabu ya mabilioni ya dola husafirishwa kwenda UAE
30 Mei 2024![Mchimbaji madini kutoka Tanzania Assia Hussein, ambaye ni mwenyekiti wa chama cha wachimbaji madini wanawake, akiangalia baadhi ya madini ya dhahabu katika soko la dhahabu mjini Geita, Tanzania Mei 28, 2022.](https://static.dw.com/image/67331513_800.webp)
Matangazo
Usafirishaji haramu wa dhahabu kutoka Afrika umeelezwa katika ripoti iliyochapishwa leo na shirika la Swissaid, linaloangazia misaada ya maendeleo na uhamasishaji.
Dhahabu ya thamani ya dola bilioni 30 ilisafirishwa mwaka 2022
Uchambuzi uliofanywa na Swissaid, umegundua kuwa jumla ya tani 435 za dhahabu, inayochimbwa zaidi na wachimbaji migodi wadogo na yenye thamani ya zaidi ya dola bilioni 30, ilisafirishwa nje ya Afrika mnamo mwaka 2022.
UAE ni kituo kikuu cha dhahabu kutoka Afrika
Swissaid imesema UAE ndio kituo kikuu cha dhahabu hiyo kutoka Afrika na kwamba muongo mmoja awali, ilipokea zaidi ya tani 2,500 za dhahabu yenye thamani ya jumla ya zaidi ya dola bilioni 115.