Dharuba yapiga Bangladesh
23 Septemba 2007Matangazo
Dhaka:
Wavuvi zaidi ya 100 hawajulikani waliko baada ya kimbunga kupiga nchini Bangladesh.Maafisa wa serikali wanasema mashua zaidi ya 15 zimezama.Mawimbi makubwa yanakorofisha shughuli za kuwaokoa walionusurika.Maafisa wa forodha huko Chittagong wamepiga marufuku safari zote za meli na mashua,hadi amri mpya itakapotolewa.