Diego Maradona amefariki dunia
25 Novemba 2020Matangazo
Gwiji la soka raia wa Argentina Diego Maradona amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 60, msemaji wake ametangaza Jumatano.
Mapema mwezi huu, Maradona aliondoka hospitali baada ya kufanyiwa upasuaji kuondoa damu iliyokuwa imeganda katika ubongo wake, huku wakili wake Matias Moria akisema ulikuwa muujiza kwamba damu hiyo iliyoganda, ambayo ingesababisha kifo chake, ilikuwa imegundulika mapema.
Katika kipindi cha miaka 20 iliyopita, Maradona amelazwa hospitali mara tatu kwa hali mbaya ya afya kutokana na utumiaji wa dawa za kulevya na kilevi. Hivi karibuni, alilazimika kukaa karantini nyumbani kutokana na janga la COVID-19.