1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaDjibouti

Djibouti kufanya uchaguzi wa rais siku ya Ijumaa

10 Aprili 2026

Uchaguzi wa rais unafanyika siku ya Ijumaa kwenye taifa hilo lenye umuhimu mkubwa wa kimkakati katika Pembe ya Afrika.

 Rais wa Djibouti, Ismail Omar Guelleh
Rais wa Djibouti Ismail Omar Guelleh ambaye ameiongoza nchi hiyo kwa miaka 27..Picha: Mohammed Dhaysane/AA/picture alliance

Rais wa Djibouti, Ismail Omar Guelleh, anatafuta nafasi ya kuiongoza nchi hiyo ya Pembe ya Afrika  kwa muhula wa sita na atachuana na mgombea mmoja tu asiye na umaarufu sana Mohamed Farah Samatar, ambaye ni kiongozi wa Chama cha Unified Democratic Center (CDU), ambacho hakina hata kiti kimoja bungeni.

Zaidi ya wapiga kura 256,000 wanatarajiwa kushiriki uchaguzi huo.  Guelleh ameiongoza nchi hiyo yenye takriban wakaazi milioni moja kwa mkono wa chuma kwa miaka 27. Nchi hiyo ndogo inahifadhi kambi na vikosi vya kijeshi kutoka Ufaransa, Marekani, China, Japan na Italia, jambo linalozalisha faida kubwa za kifedha, kiusalama na kisiasa.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW