1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Djokovic ashinda kesi dhidi ya Australia

10 Januari 2022

Huenda Novak Djokovic akashiriki mashindano ya Australian Open baada ya mahakama Australia kuamua serikali ya Australia haikuwa na sababu za kutosha za kumzuia nyota huyo kuingia nchini humo kwa ajili ya mashindano hayo.

Tennisspieler Novak Djokovic
Picha: WILLIAM WEST/AFP

Mawakili wa Djokovic walisema kwamba ana udhuru wa kimatibabu baada ya kuugua virusi vya corona hivyo hastahili kuchomwa chanjo jambo ambalo serikali ya Australia ilikataa na kumzuia tangu wiki iliyopita.

Lakini sasa mahakama hiyo imetoa amri ya kuachiwa kwa mchezaji huyo wa Tennis ila waziri wa uhamiaji wa Australia Alex hawke anatafakari iwapo aifutilie mbali visa ya Djokovic kwani kisheria anaweza kufanya hivyo licha ya amri ya mahakama, jambo litakalomaanisha kwamba Djokovic atakuwa na marufuku ya kuingia Australia kwa miaka mitatu.

Wachezaji wenzake wameanza kumuunga mkono kwa mfano kufuatia uamuzi huo wa mahakama Rafael Nadal amesema kwamba Djokovic sasa anastahili kuruhusiwa ashirike kombe la Australian Open.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW